Swahili
Surah Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya count 26
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ 
( 1 ) 
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ خَاشِعَةٌ 
( 2 ) 
Siku hiyo nyuso zitainama,
عَامِلَةٌ نَّاصِبَةٌ 
( 3 ) 
Zikifanya kazi, nazo taabani.
تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةً 
( 4 ) 
Ziingie katika Moto unao waka -
تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ آنِيَةٍ 
( 5 ) 
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
لَّيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٍ 
( 6 ) 
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
لَّا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِي مِن جُوعٍ 
( 7 ) 
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاعِمَةٌ 
( 8 ) 
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
لِّسَعْيِهَا رَاضِيَةٌ 
( 9 ) 
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ 
( 10 ) 
Katika Bustani ya juu.
لَّا تَسْمَعُ فِيهَا لَاغِيَةً 
( 11 ) 
Hawatasikia humo upuuzi.
فِيهَا عَيْنٌ جَارِيَةٌ 
( 12 ) 
Humo imo chemchem inayo miminika.
فِيهَا سُرُرٌ مَّرْفُوعَةٌ 
( 13 ) 
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
وَأَكْوَابٌ مَّوْضُوعَةٌ 
( 14 ) 
Na bilauri zilizo pangwa,
وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌ 
( 15 ) 
Na matakia safu safu,
وَزَرَابِيُّ مَبْثُوثَةٌ 
( 16 ) 
Na mazulia yaliyo tandikwa.
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى الْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ 
( 17 ) 
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
وَإِلَى السَّمَاءِ كَيْفَ رُفِعَتْ 
( 18 ) 
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
وَإِلَى الْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ 
( 19 ) 
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
وَإِلَى الْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ 
( 20 ) 
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
فَذَكِّرْ إِنَّمَا أَنتَ مُذَكِّرٌ 
( 21 ) 
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ 
( 22 ) 
Wewe si mwenye kuwatawalia.
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ 
( 23 ) 
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
فَيُعَذِّبُهُ اللَّهُ الْعَذَابَ الْأَكْبَرَ 
( 24 ) 
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
إِنَّ إِلَيْنَا إِيَابَهُمْ 
( 25 ) 
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُم 
( 26 ) 
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!